Hamad Rashid Mohammed wa ADC Aahidi Kusimama Imara Kulinda Muungano, Ataka Wanasiasa Waache Kauli za Uvunjifu

politics | Wed Oct 01 2025


Hamad Rashid Mohammed wa ADC Aahidi Kusimama Imara Kulinda Muungano, Ataka Wanasiasa Waache Kauli za Uvunjifu

Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ADC (Alliance for Democratic Change), Hamad Rashid Mohammed, ametoa msimamo thabiti wa chama chake kuhusu Muungano, akiahidi kuuimarisha na kuudumisha, huku akionya dhidi ya wanasiasa wanaotoa kauli za kuupuuza au kuuvunja.


Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni katika viwanja vya Mwenge, Makunduchi mkoani Kusini Unguja, Hamad Rashid alisema Muungano wa Tanganyika na Zanzibar umekuwa nguzo ya mshikamano na mfano wa kuigwa kimataifa, na hakuna chama makini cha siasa kinachoweza kubeza thamani yake.


"Chama chochote makini hakiwezi kubeza Muungano. Huu ndio umetuunganisha na kutufanya kitu kimoja, na leo ni mfano unaoheshimika hata kwa mataifa ya nje," alisema mgombea huyo.


Alisisitiza kuwa amani na mshikamano uliopo nchini unatokana na kuwepo kwa Muungano. Kwa sababu hiyo, aliwataka wananchi wa Zanzibar kupima kwa makini kauli zote zinazotolewa na baadhi ya wanasiasa kuhusu madai ya kuvunja Muungano, akisema kauli hizo ni za hatari kwa umoja wa taifa.


Hamad Rashid alihitimisha kwa kusema kuwa ADC iko tayari kulinda Muungano kwa nguvu zote, akiongeza: "Hatuwezi kuruhusu uvunjike, tutaendelea kuusimamia na kuudumisha," kwani Muungano umelipa heshima kubwa taifa la Tanzania.

I recommend this article.

You can participate in article recommendations up to 50 times within 24 hours.


0 comments


Messages unrelated about this certain topic may be deleted or restricted.

0/300
Loading...

The copyright for this content belongs to the copyright holder or provider. Unauthorized use may result in legal liability under copyright laws and other regulations.