Mji mkuu wa Uholanzi, Amsterdam, umeshuhudia tukio la kusikitisha la kudungwa kwa kisu ambapo watu wasiopungua watano wamejeruhiwa. Tukio hilo lilitokea mnamo tarehe 27 katika eneo la karibu na Uwanja wa Dam, ambao ni kitovu cha jiji.
Shirika la habari la taifa la NOS limeripoti kuwa mtu mmoja anayeshukiwa kuhusika na shambulio hilo amekamatwa mara moja katika eneo la tukio.
Polisi wametangaza kufunga Mtaa wa Sint Nicolaasstraat, ambao ni maarufu kwa watalii, na wanaendelea na uchunguzi kubaini mazingira kamili ya tukio hilo. Hadi sasa, nia ya mshambuliaji haijajulikana.
NOS iliripoti zaidi kuwa helikopta ya kituo cha huduma za dharura ilitua karibu na Kasri la Kifalme katika Uwanja wa Dam na kuwabeba majeruhi kwa ajili ya matibabu.
Baada ya tukio hilo, maduka yaliyoko katika mtaa uliofanyika shambulio yalifungwa, na usafiri wa treni za umeme kupitia uwanja huo ulisimamishwa.
Polisi wamewataka wananchi kuepuka eneo hilo na wamewasihi mtu yeyote aliye na picha au video za tukio hilo kuzisaidia katika uchunguzi.